RATIBA YA LIGI KUU YA NBC 2024/2025 TAZAMA HAPA


INEC RATIBA YA UBORESHAJI WAPIGA KURA 2024/2025 HAPA


INEC KUITWA KWENYE USAILI 2024/2025 TAZAMA HAPA


AJIRA MPYA KILA SIKU TAFADHALI BONYEZA HAPA


JIUNGE NASI TELEGRAM BOFYA HAPA WHATSAPP HAPA


INEC Ratiba ya Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura 2024/2025

Filed in Ajira, Habari, Makala, Michezo by on 25/07/2024
SHARE THIS POST:

JIUNGE NASI TELEGRAM BOFYA HAPA WHATSAPP BOFYA HAPA

INEC Ratiba ya Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura 2024/2025

INEC Ratiba ya Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura 2024/2025, INEC Ratiba ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Mwaka 2024/2025,NEC Timetable For Improvement Of Voter Register 2024/2025,NEC Selected Applicants NEC Jobs Tanzania 2024.

INEC Ratiba ya Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura 2024/2025

INEC Ratiba ya Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura 2024/2025, INEC Ratiba ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Mwaka 2024/2025,NEC Timetable For Improvement Of Voter Register 2024/2025,NEC Selected Applicants NEC Jobs Tanzania 2024.

Uzinduzi wa zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura utafanyika Jumamosi ya tarehe 20 Julai, 2024 Mkoani Kigoma ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (MB).

INEC Ratiba ya Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura 2024/2025

Kuelekea Uzinduzi huo hii hapa ni Ratiba Kamili ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Kwa Mikoa yote Mwaka 2024/2025.

RATIBA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA MWAKA 2024/2025 DONWLOAD PDF

UBORESHAJI WA DAFTARI

Kwa mujibu wa Kifungu cha 16 (5) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, Na. 1 ya Mwaka 2024, Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura utakuwa mara mbili kati ya kipindi kinachoanza mara baada ya uchaguzi mkuu na kabla ya siku ya Uteuzi.

Wanaohusika katika zoezi hili ni wananchi ambao: –

  1. Wametimiza umri wa miaka 18 na kuendelea ambao hawakuandikishwa hapo awali;
  2. Watakaotimiza miaka 18 kabla ya tarehe ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025;
  3. Waliojiandikisha awali na wamehama Kata au Jimbo moja kwenda jingine;
  4. Waliopoteza sifa mfano wale waliofariki kuondolewa katika Daftari;
  5. Wenye taarifa zilizokosewa wakati wa uandikishaji; na
  6. Waliopoteza au kadi zao kuharibika.

Watendaji wa Uandikishaji/ Uboreshaji

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi hutumia watendaji mbalimbali wakati wa Uandikishaji na Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. Watendaji hawa ni pamoja na:-

  1. Waratibu wa Uchaguzi wa Mkoa;
  2. Maafisa Waandikishaji;
  3. Maafisa Waandikishaji Wasaidizi;
  4. Waandishi Wasaidizi; na
  5. Mwenyesha Kifaa cha Bayometriki
INEC Ratiba ya Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura 2024/2025, INEC Ratiba ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Mwaka 2024/2025,NEC Timetable For Improvement Of Voter Register 2024/2025,NEC Selected Applicants NEC Jobs Tanzania 2024.

INEC Ratiba ya Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura 2024/2025

Mawakala wa Uandikishaji wa Wapiga Kura

Kwa mujibu wa Kifungu cha 17 (1) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, Na. 1 ya Mwaka 2024, Chama cha Siasa chenye usajili wa kudumu kinaweza kumteua mtu mmoja katika kila kituo cha uandikishaji kuwa Wakala wa Uandikishaji wa Wapiga Kura.

Wajibu/Majukumu ya Mawakala wa Uandikishaji

  1. Kufuatilia zoezi la uboreshaji na kutazama kama linazingatia Sheria, Kanuni na Maelekezo ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.
  2. Kushirikiana na Waandishi Wasaidizi kutambua wakazi wa eneo hilo na kutoa taarifa juu ya watu wasio na sifa.

Pamoja na majukumu tajwa, Mawakala wa Uboreshaji hawaruhusiwi kufanya yafuatayo:-

  1. Kuingilia shughuli za uendeshaji wa zoezi la Uboreshaji. Msimamizi wa kituo ndiye mwenye mamlaka ya mwisho juu ya nani anastahili kuandikishwa au kuboresha taarifa zake kwa mujibu wa Sheria.
  2. Kufanya kampeni za kisiasa katika kituo cha uandikishaji
  3. Kuorodhesha majina ya watu wanaojiandikisha.

Kiapo cha Kutunza Siri cha Mawakala wa Uandikishaji

Kila Wakala wa Uandikishaji kabla ya kuanza kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Sheria, ni lazima kula kiapo cha kutunza siri za taarifa za mwombaji au Mpiga Kura aliyeandikishwa. Wakala atakula kiapo mbele ya Afisa Mwandikishaji au Afisa Mwandikishaji Msaidizi. Hata hivyo, kutokuwepo kwa Wakala wa uandikishaji katika kituo cha kuandikisha Wapiga Kura hakuzuii utekelezaji wa majukumu ya Uandikishaji Wapiga Kura.

Watazamaji wa Uandikishaji

Kwa mujibu wa Kanuni za 46, 47, 48, 49, 50 na 51 (1) za Kanuni za Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura za Mwaka 2024 zilizoandaliwa chini ya Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, Na. 1 ya Mwaka 2024  Watazamaji wa ndani na kimataifa, wanaruhusiwa kutazama mchakato wa Uboreshaji utakavyofanyika katika vituo vya Uandikishaji.

Watazamaji wa Uandikishaji kabla ya kuanza kutembelea vituo vya Uandikishaji, ni lazima waombe na kupatiwa idhini ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kuwa Watazamaji.

Aidha, Watazamaji 24 watakaoruhusiwa na Tume watapewa barua za kuwatambulisha kwa Maafisa Waandikishaji na Mwongozo wa watazamaji wa zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ulioandaliwa na Tume.

Maafisa Waandikishaji watatakiwa kuwapa barua za kuwatambulisha kwa Watendaji wa vituo ambavyo watavitembelea.

Aidha, Watazamaji wa Uandikishaji wa Wapiga Kura hawapaswi kutoa maelekezo kwa Mwandishi Msaidizi katika kituo husika.

Kuweka Wazi Daftari la Awali la Wapiga Kura

Kwa mujibu wa Kifungu vya 11 (2) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya Mwaka 2024, Tume inatakiwa kuweka wazi Daftari la Awali la Wapiga Kura ili kutoa fursa kwa wananchi:

  1. Kulikagua Daftari;
  2. Kufanya marekebisho ya majina au mahali wanapoishi;
  3. Kuingiza au kufuta majina ya Wapiga Kura;
  4. Kuweka pingamizi kwa Mpiga Kura aliyeandikishwa na hana sifa za kuwemo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

Kumuwekea Pingamizi aliyeandikishwa kwenye Daftari la Awali

Kifungu cha 27 cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, Na. 1 ya Mwaka 2024,kinaruhusu Mkurugenzi wa Uchaguzi au Afisa Mwandikishaji au mtu yeyote aliyeandikishwa kuwa Mpiga Kura, kuweka pingamizi dhidi ya jina lililopo katika Daftari la Awali la Wapiga Kura. Kifungu cha 28 Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, Na. 1 ya Mwaka 2024,  kinaweka utaratibu wa kuweka pingamizi. Mtu aliyewekewa pingamizi hutakiwa kupelekewa taarifa ili aweze kutoa ufafanuzi ndani ya siku saba (7).

Kifungu cha 29 cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, Na. 1 ya Mwaka 2024 Mahakama itapaswa kutoa uamuzi wa rufaa hiyo ndani ya siku 14 tangu tarehe ya kupokea rufaa hiyo, uamuzi wa Mahakama ya Wilaya na iwapo aliyewekewa pingamizi hakubaliani na 25 maamuzi ya Afisa Mwandikishaji ya kuendelea kukataliwa kuwemo katika Daftari, ana haki ya kukata rufaa dhidi ya maamuzi Wilaya ndiyo utakuwa uamuzi wa mwisho na mtu hatoweza kukata rufaa katika Mahakama nyingine yoyote.


HISTORIA YA TUME HURU YA UCHAGUZI TANZANIA (INEC)

Mwaka 1991, aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Ali Hassan Mwinyi aliteua Tume chini ya Uenyekiti wa Hayati Jaji Mkuu Mstaafu Francis Nyalali. Madhumuni ya Tume hiyo ilikuwa ni kukusanya maoni ya wananchi juu ya kuendelea na mfumo wa chama kimoja au kuwa na mfumo wa vyama vingi vya siasa. Kutokana na ripoti ya Tume hiyo, ibara ya 3(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ilirekebishwa na kufanya Tanzania kuwa Taifa linalofuata mfumo wa vyama vingi vya siasa.

Vilevile, Sheria ya Vyama vya Siasa, (Na. 5 ya 1992) ilitungwa ili kuwezesha usajili wa vyama vya siasa. Pia, Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, (Na.1 ya 1985) na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, (Na. 4 ya 1979) zilirekebishwa ili kuondokana na mfumo wa chama kimoja na kuruhusu kufanyika kwa Uchaguzi chini ya mfumo wa vyama vingi vya siasa. Baada ya marekebisho hayo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilianzishwa tarehe 13 Januari, 1993.

Aidha, mwaka 2021 ulifanyika Mkutano wa Wadau wa Kujadili Hali ya Demokrasia ya Vyama Vingi vya Siasa nchini Tanzania. Pamoja na mambo mengine, mkutano huo ulitoka na azimio la kuboresha mfumo wa uchaguzi nchini. Hivyo, tarehe 23 Desemba 2021, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan aliunda kikosi kazi cha kutathmini hali ya demokrasia ili kutoa mapendekezo ya kuboresha masuala ya demokrasia na hali ya kisiasa nchini.

Kikosi kazi, kilitoa mapendekezo ya kufanyika kwa maboresho ya Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292. Maboresho hayo yalisababisha kutungwa kwa Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Na. 2 ya Mwaka 2024 na Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya Mwaka 2024. Kufuatia kutungwa kwa Sheria hizo, jina la Tume ya Taifa ya Uchaguzi lilibadilika na kuwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imeanzishwa kwa mujibu wa ibara ya 74(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Kwa kuzingatia masharti ya ibara ya 74(7) na (11) ya Katiba na kifungu cha 6(1) cha Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Na. 2 ya Mwaka 2024, Tume ni idara huru inayojitegemea na inafanya maamuzi yake rasmi kuhusu utekelezaji wa majukumu yake kwa vikao. Katika kutekeleza majukumu yake ya kikatiba, Tume haitalazimika kufuata amri au maagizo ya mtu yeyote au idara yoyote ya Serikali au maoni ya chama chochote cha siasa.

PATA NYIMBO ZOTE MPYA BONYEZA HAPA

MATANGAZO YA BIASHARA WASILIANA NASI KUPITIA nijuzehabariblog@gmail.com

SHARE THIS POST:

Tags: , , , , ,

Comments are closed.